HUDUMA YA ULTRASOUND

Posted on: November 19th, 2020

Kipimo cha ultrasound kinamsaidia daktari kuona kama kuna tatizo katika ogani, mishipa na tishu bila kufanya upasuaji. Tofauti na tekinolojia nyingine, ultrasound haitumi mionzi, ndio maana ni njia inayopendekezwa kwaajili ya kuangalia ukuaji wa kijusi kipindi cha ujauzito. Wakati wa kufanya kipimo cha ultrasound ni muhimu sana kwa wajawazito wengi- ni mara ya kwanza unapoweza kumuona mtoto wako. Unaweza kuona mikono, miguu na sehemu nyingine za mwili kulingana na lini kipimo kitachukuliwa na mkao wa mtoto wako tumboni. Utaweza pia kujua jinsia ya mtoto wako.

Wanawake wemgi wanafanya kipimo cha ultrasound katika kipindi cha pili cha miezi mitatu ya ujauzito (second trimester) wiki 18-20 ya ujauzito. Baadhi wanafanya katika kipindi cha kwanza cha miezi mitatu ya ujauzito (kabla ya wiki ya 14 ya ujauzito). Idadi ya vipimo vya utrasound na muda unaweza tofautiana kwa wanawake wenye aina fulani ya matatizo ya kiafya kama asthma na kisukari.

Kuna Tofauti Gani Kati ya Kipimo cha Ultrasound na X-ray?

Ultrasound inatumia mawimbi ya sauti na mwangwi kutoa picha hai, kama video.

X-rays ni njia rahisi na haraka kwa mtaalamu wa afya kutumia kuona viungo vya ndani ya mwili na hali ya mifupa. X-rays zinatumia mionzi kupiga picha ya ogani za ndani ya mwili, na mionzi hiyo ina madhara makubwa kwa afya ya binadamu. Picha zinazopigwa zinafanana na kivuli cha mwili wa ndani wa binadamu.

Kwanini kipimo cha Ultrsound Kinafanyika?

Vipimo hivi vitampatia mama mtarajiwa nafasi ya kumuona mtoto wake ambaye hajazaliwa. Lakini pia kipimo hichi kina kazi nyingine.

Daktari wako atakutaka ufanye kipimo hich kama utakua na maumivu, kuvimba au dalili nyingine itakayo hitaji uchunguzi wa ogani za ndani ya mwili. Ultrasound inaweza kuangalia sehemu za mwili kama vile: kibofu cha mkojo, ubongo (wa mtoto), macho, figo, ini, ovari, bandama, uterasi, korodani, na mishipa ya damu.

Copyright ©2022 CHATOZRH . All rights reserved.